Kongamano la kimataifa la Kiswahili lazinduliwa Zanzibar

     

Lugha ya kiswahili imekuwa 
lugha rasmi ya serikali na taifa la Tanzania  hutumika katika shule za msingi  lakini shule za upili na vyuoni hutumika katika shughuli za kawaida na ligha ya   Kiingereza hutumika kufundishia. 
     Mnamo tarehe 15 Februari 2015 rais mstaafu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete alitangaza mpango wa kubadilisha lugha ya elimu nchini kwa kutumia Kiswahili kwenye ngazi zote hadi shule za sekondari na chuo kikuu hii ikiwa ni katika kukuza na kuenzi lunga ya kiswahili
      Leo hii rais wa serikali ya mapinduzi ya  Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, anazindua kongamano la kimataifa la Kiswahili linalofanyika katika viwanja vya Baraza la Wawakilishi la zamani mjini Unguja.
    Taarifa iliyotolewa  na Mwenyekiti wa Baraza la Kiswahili Zanzibar (Bakiza), Mohamed Seif Khatib imesema kuwa kongamano hilo la siku mbili litajadili mada 100 zitakazowasilishwa na wageni, zikiwamo makala maalumu zinazohusiana na lugha ya kiswahili
       Mwenyekiti huyo amebainisha tamasha hilo linatazamiwa kuwa na  washiriki wapatao 100 wakiwamo wataalamu wa Kiswahili wa ndani na nje ya nchi, taasisi za kiraia, wataalam na wanafunzi kutoka vyuo vikuu pamoja na wananchi.
       Kwa upande wake katibu mtendaji wa baraza hilo, Mwanahija Ali Juma aliwataka wananchi kuchangamkia fursa ya kongamano hilo kwa kushiriki ili nao waweze kuongeza utaalamu zaidi katika kutumia misamiati ya lugha yao.

1 comment:

  1. The Casino: What's on the card?
    A few 이천 출장마사지 words to say to 삼척 출장안마 casino players: of poker chips that are dealt out to 당진 출장안마 the casino floor to a and then a large amount of cash in 삼척 출장마사지 the name of the 전라북도 출장샵 card.

    ReplyDelete