Shashi Kapoor atakumbukwa kama mwigizaji maarufu katika filamu mbalimbali maarufu kutoka India na nje ya india kama vile Deewar na Kabhie Kabhie,
Amekuwa akiugua kwa muda na siku za karibuni alikuwa amelazwa hospitali ya Kokilaben Dhirubhai Ambani ya mjini Mumbai hadi mauti yalipomkuta akiwa na umri wa miaka 79.
Taarifa ya kifo chake ilipatikana kwa mujibu wa mpwa wake Randhir Kapoor ambaye ameliambia jarida la Press Trust of India kwamba Kapoor amekuwa akitatizwa na figo kwa miaka mingi.
Shashi Kapoor alikuwa amemuoa Jennifer Kendal ambaye ni mwigizaji mwingereza na kwa pamoja walifanikiwa kuanzisha ukumbi maarufu wa sanaa Mumbai ujulikanao kwa jina la Prithvi mwaka 1978.
Shashi Kapoor atakumbukwa kwa filamu zake maarufu kama vile Haseena Maan Jayegi (1968) Ek Shriman Ek Shrimati (1969) Kanyadan (1968) Pyar Ka Mausam (1969) na nyinginezo
No comments:
Post a Comment