Yaliyomuudhi Mwigulu mwaka 2017 ni haya


Mbunge wa Iramba magharibi na waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi mheshimiwa  Mwigulu Nchemba amesema kwamba miongoni mwa matukio  yaliyomuudhi sana mwaka 2017 ni pamoja na tukio la kushambuliwa kwa Mbunge wa Singida Mashariki kwa tiketi ya chama cha demokrasia na maendeleo Mh Tundu Lissu.

Mbali ya tukio la kushambuliwa kwa Lissu  mauaji ya wananchi na Askari huko Kibiti pia ni jambo jingine ambalo lilitikisa vichwa vya habari nchini Tanzania.

Mh. Mwigulu Nchemba ambaye ni waziri wa mambo ya ndani ya nchi  ameyasema hayo wakati  akiongea na waandishi wa habari mkoani Dodoma.


Waziri huyo pia ametoa mwelekeo wa wizara ya mambo ya ndani ya  nchi kwa mwaka mpya wa 2018 nini kama wizara wamejipanga kufanya.

No comments:

Post a Comment