Aliyoyasema JPM baada ya Babu Seya kumtembelea ikulu


Mwanamuziki maarufu Nguza Viking almaarufu kama Babu Seya aikiongozana na wanawe leo hii wamemtembelea Rais wa jamhuri ya muungano Dkt John Magufuli ikulu kwa lengo la kumshukuru baada yake kuwaachilia huru kwa msamaha wa rais desemba 9 mwaka huu.

Hapo awali Nguza Viking pamoja na mwanae walikuwa wanatumikia kifungo cha maisha jela hadi walipotoka kwa msamaha wa raisi desemba 9 mwaka huu

Hivyo basi kama sehemu ya shukrani leo hii wameamua kumtembelea Dkt Magufuli ili waweze kutoa shukrani zao ambapo mbali na mazungumzo mengine Dkt magufuli amewaambia kuwa shukrani za pekee zimwendee Mwenyezi Mungu kwani yeye ndiye husamehe.



No comments:

Post a Comment