Kichanga chaokotwa mkesha wa mwaka mpya 2018


Kila mtoto anayezaliwa anatamani aishi hivyo jamii inapaswa kuwalinda watoto.( Picha na mtandao)
Mwaka unapoanza kila mtu hujawa na fura na kumshukuru Mungu kwa kuweza kuuona mwaka mwingine.
Wengi wetu hufurahia afya njema pamoja na uhai tunaokuwa nao lakini hali imekuwa tofauti katika mkesha wa mwaka 2018 kwani  mtoto mchanga wa kiume anayekadiriwa kuwa na umri wa siku tatu ameokotwa akiwa amekufa baada ya kutupwa  kwenye kichaka eneo la Tandale na watu wasiojulikana.
 Kwa mujibu wa Muuguzi wa zamu wa Hospitali ya Mwananyamala Bi. Jasmine mwili wa  mtoto huyo umeokotwa na jeshi la polisi na kwa sasa  uhifadhiwa katika hospitali hiyo.
Muuguzi huyo amesema mbali ya tukio hilo la kinyama  jumla ya watoto saba wamezaliwa usiku wa kuamkia mkesha wa mwaka mpya wa 2018.

No comments:

Post a Comment